Taarifa zilizoenea katika mitandao ya
kijamii hasa kuanzia jana zimeeleza kuwa mwanamziki huyo ameachana na
mziki na kuamua kumrudia Mungu.
Akizungumza, mmiliki huyo wa bendi ya
Jahazi Modern Taarab amethibitisha kuwa taarifa hizo ni za kweli:
“Nashangaa taarifa hizi zinasemwa leo. Ni suala la muda mrefu… takribani
miezi miwili iliyopita na sababu ni kuwa nimeamua kumrudia Allah,” Mzee
Yusuf alisema.
Mwimbaji huyo wa huyo wa taarabu mzaliwa
wa Zanzibar alipoulizwa kuwa ni suala gani lililomsukuma hata achukue
maamuzi hayo magumu, alijibu kwa kifupi, “ndivyo tunavyofundishwa na
viongozi wa dini.”
Yusuph aliyetamba na vibwagizo kama
“Nichumu, nikisi….mwaaaa,” katika baadhi ya nyimbo zake, amesema familia
yake imeupokea uamuzi wake kwa mtazamo chanya na kwamba inamuunga
mkono.
“Kwa sasa nitaimba kaswida zenye mafundisho ya dini,” amesema nyota huo huku akiahidi kufanya mkutano rasmi kuelezea suala hilo.
Mfalme huyo aliyeonekana kuwa ni gwiji
wa taarabu ya kisasa (modern taarab) amezaliwa visiwani Zanzibar mwaka
1977. Aidha amejihusisha na sanaa nyingine kama maigizo.
Ni mshindi wa tuzo katika tasnia ya muziki wa taarab zikiwemo ya Kilimanjaro Music Award 2014-15.
- Kikundi bora cha mwaka taarab – Jahazi Modern Taarab
- Mtunzi bora wa mwaka taarab- Mzee Yussuf
- Mwimbaji bora wa kiume taarab – Mzee Yussuf
Maamuzi Magumu Aliyoyafanya Mzee Yusuf, Aachana na Uimbaji wa Taarab
4/
5
Oleh
hamisi shehe