Showing posts with label NEWS. Show all posts
Showing posts with label NEWS. Show all posts

Friday 17 November 2017

MSIBA WA NDIKUMANA WAMTESA UWOYA


Staa wa Bongo, Irene Pancras Uwoya.
WAKATI kifo cha aliyekuwa mume wa staa wa sinema za Kibongo, Irene Pancras Uwoya, Hamad Ndikumana Katauti (39), raia wa Rwanda kilichotokea usiku wa kuamkia Jumatano wiki hii, kikiibua utata kutokana na mshtuko wake, hali hiyo kwa mkewe huyo inafananishwa na kile kilichomkuta mwanamama Zarinah Hassan Tiale ‘Zari The Boss Lady’ kwa mumewe, Ivan Ssemwanga ‘Don Ivan’ miezi kadhaa iliyopita.
VYANZO VYA RWANDA
Kwa mujibu wa vyanzo kutoka nchini Rwanda, chanzo cha kifo cha mume wa Uwoya ni matatizo ya moyo huku kikishangaza kwani jana yake (Jumanne) alikuwa fiti akiendelea na kazi zake kama kawaida.
Hadi anakutwa na umauti, Ndikumana alikuwa Kocha Msaidizi wa Timu ya Rayon Sports ya Rwanda ambapo saa kadhaa kabla ya umauti alikuwa akifanya mazoezi na wachezaji wake.
Akithibitisha kutokea kwa kifo hicho, Afisa Habari wa Rayon Sports, Gakwaya Olivier alisema kuwa, Ndikumana alifariki kwa kile kilichosadikiwa kuwa ni ugonjwa wa moyo.
UTATA
Utata wa kifo cha Ndikumana unaelezwa kutokana na namna kifo hicho kilivyotokea ghafla.
“Alisikia maumivu makali kifuani, akaomba soda ya baridi, wakamletea na alipomaliza kunywa kidogo tu, alitapika kisha akaishiwa pumzi na ndipo akakata kauli,” alisema afisa habari huyo.
Akiwa katika pozi.
NDOA YA UWOYA NA DOGO JANJA YATAJWA
Wakati simanzi hiyo ikizua mjadala mkali, baadhi ya watu walidai kuwa, matatizo hayo ya moyo huenda yalitokana na msongo kufuatia mkewe huyo ambaye alikuwa hajampa talaka kudaiwa kufunga ndoa na msanii wa Bongo Fleva, Abdulaziz Chende ‘Dogo Janja’ hivi karibuni.
Wachambuzi wa matukio ya mastaa Bongo walieleza kuwa, baada ya stori za Uwoya na Dogo Janja kuibua mjadala mzito, Ndikumana alikuwa akiposti maneno ya mafumbo mitandaoni kabla ya kumtambulisha mpenzi wake mpya.
UWOYA YAMKUTA YA ZARI
Ilisemekana kwamba, kifo cha mume huyo wa Uwoya kinatengeneza mazingira kama yale ya kifo cha mume wa Zari, Ivan ambaye naye alikutwa na umauti kutokana na matatizo ya moyo na baadaye kufuatiwa na mama yake.
NDIKUMANA KAMA IVAN
“Kifo cha Ivan na chenyewe ilidaiwa kilitokana na msongo baada ya Zari kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na mtu mwingine kama ilivyo kwa Ndikumana baada ya Uwoya kudaiwa kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na Dogo Janja,”
kilisema chanzo hicho na kuongeza;
“Kilichomkuta Uwoya kinafanana kabisa na kile kilichotokea kwa Zari kwani utagundua kuwa wote waliingia kwenye mapenzi na wasanii wa Bongo Fleva.
Irene Pancras Uwoya na Hamad Ndikumana Katauti (39) enzi wakiwa pamoja.
HAKUKUWA NA TALAKA
“Kama hiyo haitoshi, wote walikuwa hawajapewa talaka na waume zao na hata ugonjwa uliowasababishia waume zao umauti ni ugonjwa wa moyo.
“Pia wote vifo vyao vilikuwa vya ghafla kwani hawakuripotiwa kuwa wanaumwa.
BADO WALIWAHITAJI
“Kibaya zaidi wote walisharipotiwa kuwa wapo kwenye hali mbaya kutokana na kutoswa na wake zao ilihali wakiwa bado wanawahitaji.
“Ivan alikuwa akimbembeleza Zari kumrudia kama ilivyokuwa kwa Ndikumana ambaye miezi
kadhaa iliyopita alikaririwa akisema kuwa, amekuwa akimuomba Uwoya arudi kwake waendelee na maisha hasa katika suala la kumlea mtoto wao wa kiume aitwaye Krish.
Kwa upande wake, Ivan alikutwa na umauti Mei 30, mwaka huu ambapo katika ndoa yake na Zari, walijaliwa watoto watatu wa kiume, Pinto, Didy na Quincy.
MAMA UWOYA AANIKA SIRI
Kwa upande wake mama Uwoya, Naima Uwoya alianika siri ya kushangaza juu ya mwanaye huyo na Ndikumana ambapo alisema kuwa, alihangaika mno kurudisha uhusiano wa wawili hao lakini ikashindikana.
Mama Uwoya alisema kuwa, katika kurejesha ndoa hiyo, alikwenda hadi nchini Israeli kwa ajili ya kufunga na kumuomba Mungu ili wawili hao wamalize tofauti zao na aliamini ipo siku mambo yangekuwa sawa, lakini ndiyo hivyo Mungu naye alikuwa na mipango yake.
MAZISHI YA NDIKUMANA YATIKISA
Ndikumana alizikwa Jumatano iliyopita nchini Rwanda ambapo mazishi yake yalitikisa kutokana na uwepo wa ndugu na marafiki wengi waliojitokeza katika mazishi hayo.
Uwoya alishindwa kwenda kumzika kwa kile kilichoelezwa na watu wake wa karibu kuwa alikuwa jijini Dar na ilikuwa ni ghafla mno hivyo leo (Ijumaa) anatarajiwa kwenda kuhani msiba nyumbani kwa Ndikumana jijini Kigali, Rwanda akiongozana na wasanii wenzake wa Bongo Muvi.
TIMU ALIZOCHEZEA NDIKUMANA
Hadi anakutwa na umauti, Ndikumana aliyezaliwa Oktoba 5, 1978, aliwahi kuzichezea timu mbalimbali zikiwemo Rayon Sports na Timu ya Taifa ya Rwanda kuanzia mwaka 1998 na kuwa nahodha wa muda mrefu wa timu hiyo iitwayo Amavubi.
Pia alicheza soka la kulipwa Ulaya katika Timu za Gent na Anderlecht za Ubelgiji, Omonia Nicosia na Limassol za nchini Cyprus kabla ya kumalizia soka lake la uwanjani akiwa na Stand United ‘Chama la Wana’ ya nchini Tanzania.
TULIKOTOKA
Julai 11, 2009, Ndikumana alifunga ndoa na Uwoya katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph jijini Dar kabla ya ndoa yao kuvunjika rasmi miaka minne iliyopita.

Source: global publishers

HIKI NDO ALICHOANDIKA MANGE KIMAMBI KUHUSU HUKUMU YA LULU

newzzzzzzzz..... Lulu amekutwa na hatia ya kuuwa bila kukusudia na amehukumiwa miaka miwili jela.......
.
.
.
Dah huyu jaji anawaza kama mimi posti yangu niliyoposti masaaa mawili yaliyopita nilisema ningekuwa jaji ningemkuta na hatia ila ningempa adhabu ndogo mwaka mmoja au miwili jela.......
.
.
Jaji ametenda haki....
.
.
Sio kama nimefurahi Lulu kafungwa nilichotaka ni kuona hakuna double standards, nilitaka kuona haki inatendeka. Na Lulu ana deserve hiyo miaka 2 jela labda itampa muda wa kufikiria how her actions affected Mama Kanumba na familia yake. Labda akitoka atakuwa more humble......
.
.
.
Lakini still mwanasheria wa serikali achukulie hatua za nidhamu na afukuzwe kazi!! Alijaribu sana kusabotage kesi ili amsaidie mtuhumiwa......
.
.
PS: December Magu anatoa misamaha kwa wafungwa, sidhani kama atawasahau wafungwa wa kumpa kiki ya kufungia mwaka kama Lulu na kina Babu Seya maana ile barua ya kina Baba Seya had Bashitel written all over it."

Million 900 INAPENDEZA ADATA KWA WEMA SEPETU

BILIONEA wa nyumba za Lugumi, Dkt Louis Shika amemfungukia ‘Tanzania Sweetheart’, Wema Issac Sepetu kuwa ni staa ambaye anamkubali ukiachana na huyo kwa upande wa muziki Ray C ni mmoja wa mwanadada ambaye anamkubali kupitia nyimbo yake ya nataka niwe na wewe

Wednesday 1 November 2017

LULU AFANYIWA MAOMBI ZIKIWA ZIMESALIA SIKU CHACHE HUKUMU KUTOLEWA


Zikiwa zimesalia siku 12 tu kabla ya hukumu yake kusomwa kufuatia kesi yake ya kuua bila kukusudia inayomkabili, taarifa zinasema maombi na sala zimekua zikitikisa nyumbani kwa msanii Elizabeth Michael ‘Lulu’.
Mtu wa karibu wa msanii huyo aliyeomba hifadhi ya jina lake, alilidokeza Risasi Mchanganyiko kuwa, baada ya kesi hiyo kufikia katika hatua ya hukumu, hivi sasa kila siku maombi yanafanyika asubuhi, mchana na jioni, kwani kwa hali ilivyo hivi sasa, kila kitu kimo mikononi mwa Mungu.
HISTORIA YA LULU: Elimu Yake, Alivyokutana na Kanumba, Familia Yake na Kila Kitu Kuhusu Yeye!!!
“Si Lulu, si Mama yake, si ndugu zake, kila mmoja anaomba kwa muda wake, wakati mwingine kwa pamoja, au mmoja mmoja, wanachojua wao hatima ya kila kitu ipo mikononi mwa Mungu, ndiyo maana sala zinaelekezwa kwake,” alisema mtu huyo.
Lulu anashtakiwa kwa kosa la kumuua bila kukusudia, aliyekuwa mpenzi wake, Steven Kanumba, katika tukio lililotokea nyumbani kwa msanii huyo, Sinza Vatican mwaka 2012.
Baada ya kusikilizwa kwa ushahidi wa Jamhuri, upande wa utetezi na wazee wa mahakama, sasa hukumu hiyo itasomwa Novemba 13, mwaka huu katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam na Jaji Sam Rumanyika.

PREZOO ADATA KWA AMBER LULU


MWANA-MUZIKI na muuza sura kwenye video mbalimbali za wanamuziki wa Bongo Fleva, Lulu Eugen ‘Amber Lulu’ amelewa na sifa anazomwagiwa na ‘mpenzi’ wake mpya, Prezoo.
Amber Lulu alisema ana furaha ya ajabu kutokana na video aliyoiachia Prezoo akimsifia kwamba anampenda, ni mzuri na ana roho nzuri, achilia mbali kuwa ameshamt-ambulisha kwa mama yake.
“Najisikia vizuri sana kusifiwa na Prezoo maana mtu ukikubalika lazima ufurahi kwa kweli, ni mtu wangu wa karibu na tuna mpango wa kufanya kazi pamoja pia, kuhusu uchumba na kutambulishwa kwa mama yake hilo kwa sasa ni siri kidogo ila siku ikifika tutaweka wazi kila kitu,” alisema Amber Lulu.

Tuesday 31 October 2017

NDUGAI: SIJAPATA BARUA YA KUJIUZULU KWA NYALANDU, HUO NI UMBEA


SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai, amesema kwamba hana taarifa za kujiuzulu kwa mbunge wa Singida Kaskazini Lazaro Nyalandu na wala hiyo barua bado haijamfikia, amekiita kitendo alichokifanya ni umbea.
Job Ndugai ameyasema hayo leo alipokuwa akizungumza na chombo kimoja cha habari nchini (jina tunalo) na kusema kwamba Lazaro hakupaswa kutangaza hivyo kabla ya kuhakikisha barua imemfikia.
Pamoja na hayo Spika Ndugai amewataka wabunge wengine kuacha kuwashwa washwa na kufanya mambo ambayo ameyaita ni ya umbea.

Source: globe publishers

SCORPION AKUTWA NA KESI YA KUJIBU MAHAKAMANI


Scorpion.
Mahakama ya Wilaya ya Ilala imemkuta mshtakiwa Salum Njwete, maarufu kwa jina la ‘Scorpion’ anayekabiliwa na shtaka la unyang’anyi wa kutumia silaha na kujeruhi ana kesi ya kujibu na anatarajiwa kuanza kujitetea, Novemba 14, mwaka huu.
Uamuzi huo umetolewa leo Oktoba 31/2017 na Hakimu Mkazi Flora Haule wa mahakama hiyo baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa na zaidi ya mashahidi kumi walioletwa mahakamani pale na upande wa Mashtaka.
Kabla ya kutolewa uamuzi huo, Hakimu Haule alimkumbushia mshtakiwa mashtaka yake. Baada ya uamuzi huo kutolewa, mshtakiwa Scorpion amedai kuwa atajitetea kwa kiapo na pia atakuwa na mashahidi wawili ambao walitoa ushahidi upande wa mashtaka.
Hata hivyo, upande wa mashtaka ukiongozwa na wakili Ester Kyala ulipinga hoja hiyo na kudai kuwa mshtakiwa huyo hawezi kutumia mashahidi ambao wamekwisha toa ushahidi wao kwa upande wa Jamhuri na kama anaweza atafute mashahidi wengine.
Kutokana na pingamizi hilo Scorpion amedai atajitetea mwenyewe na pia akaomba mahakama itumie pia ushahidi wa wale mashahidi wawili. Kufuatia hayo kesi hiyo imeahirishwa hadi November 14 mwaka huu. Mshtakiwa amerudishwa rumande kwa kuwa makosa anayoshtakiwa nayo hayana dhamana.
Katika kesi hiyo, Njwete anakabiliwa na mashtaka mawili ambayo ni unyang’anyi wa kutumia silaha na kumjeruhi Said Mrisho kwa kumchoma kisu sehemu mbalimbali za mwili zikiwemo, tumboni na mabegani na kisha kumtoboa macho kitendo anachodaiwa kutenda Septemba 6, mwaka jana katika eneo la Buguruni Sheli, jijini Dar es Salaam. Pia, anadaiwa kumwibia mali yenye thamani ya Sh 476,000/-‎

Source:globe publishers

Monday 30 October 2017

Uchawi Wamtesa Mobetto



WAKATI sakata lake la kuzaa na mtoto wa pili na mwanaume mwingine likiwa bado linarindima, umati wa watu ulikusanyika nyumbani anakoishi, Mbezi Jogoo jijini Dar es Salaam wiki iliyopita baada ya kudaiwa kukutwa kwa vitu vinavyodhaniwa kuwa ni vya kishirikina, Risasi linathibitisha.
Awali chanzo kimoja cha uhakika kilipiga simu chumba cha habari na kuelezwa kuwa kuna vitu vinavyotia shaka katika nyumba hiyo hivyo kutaka kwenda kuona vilikuwa ni nini.
“Jamani kuna vitu hapa havieleweki kwa kweli, ni kama uchawi si uchawi, labda mngefika mara moja muone, maana sidhani hata wenyewe kama wanajua kuhusu hili jambo,” kilisema chanzo hicho ambacho kilikataa kutaja jina lake.
Mara baada ya kufika katika nyumba hiyo, Risasi Mchanganyiko liliweza kuona vitu vilivyo-fungwa katika kabrasha, vikiwemo nazi, ndizi na dalili zote za mambo ya kishirikina.
Baada ya kuona vitu hivyo, waandishi wetu waligonga geti la nyumba hiyo na wenyeji walipotoka, waliulizwa kama wanajua kilichomo ndani ya kabrasha. Akionyesha kushtushwa, msichana aliyekutwa alipiga simu kwa Mobeto na mama yake kuwafahamisha, ambao nao walieleza kuwa wangefika hapo muda mchache unaofuata.
Mobeto alikuwa wa kwanza kuwasili eneo la tukio na baada ya kuelezwa kilichokutwa nje ya nyumba yake, alikuja juu akimtuhumu mwandishi kuwa ndiye anahusika na vitu hivyo, jambo lilisobababisha watu kujaa.
Mwenyekiti wa serikali ya mtaa ambaye jina lake halikupatikana mara moja aliitwa na baada ya kusikiliza maelezo ya pande zote mbili, alimchukua mwandishi kwa maelezo ya kwenda naye katika vyombo vya usalama, lakini alipotoweka eneo hilo, alimwachia, akimweleza kuwa hakuwa na kosa kwa vile aliitwa na watu hivyo alikuwa akitekeleza wajibu wake.
Chanzo Global Publishers

Picha Nyingine za Wema Sepetu Akiwa na Bwana ake Bafuni zavuja


Mrembo mwenye mvuto wa kipekee Bongo, Wema Abraham Sepetu ‘Madam’ ameendelea ‘ku-shine’, safari hii zimevuja picha mpya akiwa bafuni na mpenzi wake aitwaye Bakari Kila.
Chanzo makini kilinyetisha kuwa, licha ya Bakari kuwa nyuma ya nondo kwa msala wa madawa ya kulevya Mombasa, nchini Kenya, bado ana ubuyu wa picha mpya za Wema wakioneshana mahaba na mpenzi wake huyo wakiwa bafuni.
“Achana na skendo ya unga inayomtafuna bwana wa Wema, sahau kabisa kuhusu zile picha zilizovuja Wema akiwa na Bakari, mimi ninazo picha nyingine mpya wakiwa bafuni.
“Yani ni full mahaba, Wema anaonekana akiwa ametinga kanga moko (moja), amemkumbatia Bakari huku akimpiga busu motomoto,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:





“Kuna moja Wema anambusu Bakari shavuni lakini kuna nyingine anambusu mdomoni kabisa kama njiwa vile tena wakiwa kwenye hisia kali za kimalovee. Madam hana habari tena yeye inaonesha ndiye aliyekuwa anapiga picha.”
Bakari anatajwa kuwa na mkwanja mrefu kiasi cha kumtuliza Wema hadi akaacha ‘makeke’ ya mjini, kabla jamaa huyo hajataitiwa kwa madawa ya kulevya nchini Kenya.
Global Publishers

Kwa Mara ya Kwanza Dogo Janja Afunguka Kuhusu Ndoa Yake na Irene Uwoya





HABARI zilizoenea katika mitandao ya kijamii ni kwamba msanii wa muziki wa Hip Hop nchini, Dogo Janja, amefunga ndoa kimyakimya na mnyange wa filamu, Irene Uwoya.
Baada kuenea kwa uvumi huo, mtandao wa Global Publishers ulifuatilia kujua ukweli juu ya ndoa hiyo iliyowashitua wengi.
Hatua ya kwanza jana ni pale mwandishi wa mtandao alipowaendea wahariri wa Magazeti Pendwa ya Global Publishers yanayohusiana na habari za wasanii wa Bongo Muvi, Bongo Fleva na wengineo ambapo walijibu kwamba walikuwa wamemtafuta msanii Hamad Aly ‘Madee’ aliyewajibu kwamba alikuwa hajui chochote kuhusu suala hilo.
Msanii wa muziki wa Hip Hop nchini, Dogo Janja.
Mambo hayakuishia hapo kwani wahariri haohao walipowasiliana na Dogo Janja alijibu kwamba na yeye hakujua kinachoendelea.
Mwishoni wahariri wakamalizia kwa kuongea kwenye simu na Irene Uwoya ambapo alipopokea aliulizwa kuhusu suala hilo la kufunga ndoa na Dogo Janja. Jibu la kwanza la mrembo huyo lilikuwa ni: “Mimi ni wa kuolewa? Na nitaolewa na nani? Na iweje niolewe na nyie Global msijue?”
…Alichokisema Madee kwenye akaunti yake ya Instagram.
Baada ya kuyasema hayo, muigizaji huyo mahiri wa filamu alimalizia kwa kusema kwamba yote hayo yalikuwa ni muvi ambayo alisema itatokea hivi karibuni.
Leo, Jumapili, mwandishi wa mtandao wetu aliwatafuta tena Madee, Dogo Janja na Irene Uwoya ili kujua iwapo walikuwa wanaendelea na msimamo wao kama walivyowaambia wahariri wetu.
Mambo yalianzia kwa Madee aliyesema ni kweli Dogo Janja amefunga ndoa ila hakutaja alikuwa amefunga ndoa na nani. Mwanamuziki huyo aliye na makazi yake Manzese jijini, alimalizia kwa kuupa mtandao huu namba za simu za Dogo Janja ili uongee naye.
Irene Uwoya akiwa katika pozi.
Kilichofuatia ni mtandao kumpigia simu Dogo Janja aliyeipokea na kubadilishana salam na mtandao huu lakini ghafla alinyang’anywa simu na Uwoya aliyesema kwamba ni kweli ‘bwana mdogo’ huyo alikuwa ameoa.
Hata hivyo, hakutaja kama ni yeye aliyekuwa ameolewa, lakini aliongeza kwamba: “Tafadhali tuacheni msitusumbue!”
Mpaka tunakwenda mtamboni, maelezo ya wahusika wote yalikuwa hayajaonyesha moja kwa moja kwamba ndoa hiyo kweli ilikuwa imefungwa baina ya wawili waliotajwa.
Chanzo Global Publishers

Thursday 18 August 2016

Ni kosa kumwangalia mwanamke kwa sekunde 14 nchini India

Watumiaji wa mitandao ya kijamii wamelalamika kuhusu tamko la afisa mmoja aliyesema kuwa ni kinyume na sheria kumuangalia mwanamke kwa zaidi ya sekunde 14 katika jimbo la Kerala nchini India.
http://hamisishehe.blogspot.com/2016/08/watumiaji-wa-mitandao-ya-kijamii.html
Hakuna sheria kama hiyo nchini India lakini afisa huyo Rishiraj Singh ambaye ni kamshna amesema kuwa kumuangalia mwanamke kwa mda mrefu kunaweza kukutia mashakani.
Watu mitandaoni wanauliza itakuwaje iwapo mwanamume atafunga jicho mara moja na kulifungua akimwangalia mwanamke wakiongezea kuwa huenda bei ya miwani ya kujilinda dhidi ya jua ikapanda.
Lakini wengine wanasema kuwa bwana Signh amezua hoja nzuri sana kuhusu usalama wa wanawake.
”Mtu anaweza kushtakiwa kwa kumuangalia mwanamke kwa sekunde 14”,alisema bwana Singh katika eneo la Kochi siku ya Jumamosi.
Tamko hilo lililofanywa katika kanda ya video limesambaa katika jimbo hilo na kuzua ucheshi miongoni mwa mitandao ya kijamii.
Source:BBC

Hili ndilo jina la ngoma mpya ya Alikiba?

Baada ya kuonjesha kile ambacho tutakiona kwenye video ya ngoma yake mpya, Alikiba anaweza akawa ametupa jina la wimbo huo.


http://hamisishehe.blogspot.com/2016/08/hili-ndilo-jina-la-ngoma-mpya-ya-alikiba.html
Add caption
Alikiba akiwa na warembo watakaoonekana kwenye video ya ngoma yake mpya
Mkali huyo wa Aje, ameanza kutumia neno #Kajiandae kwenye post zake mpya, huku kukiwa na uwezekano mkubwa kuwa likawa ndio jina la ngoma hiyo.
Hata hivyo bado haijulikani iwapo Kiba alienda Afrika Kusini kushoot video mbili au moja kwasababu hivi karibuni alidai kuwa alishoot video ya version ya Aje akiwa na rapper wa Nigeria, M.I.
Yeye pamoja na msanii mwenzake wa Rockstar4000, Barakah Da Prince walikuwa nchini humo kushoot video zao mpya

Wednesday 17 August 2016

Darassa adai video ya ‘Too Much’ ilimtoa jasho

Rapper ambaye anafanya vizuri kwa sasa na ngoma yake, ‘Too Much’ Darassa, amesema video ya wimbo huo ilimtoa jasho


http://hamisishehe.blogspot.com



Akiongea na kipindi cha Funiko Base cha Radio 5, Darassa alisema imemchukua muda mwingi na pesa nyingi kuikamilisha video hiyo kwakuwa alitaka kufanya kitu kikubwa.
“Too Much kwangu ni video kubwa na imetucost,imetuchukua muda,imetuumiza hapa ninavyoongea hakuna tulichobakiwa nacho zaidi ya nguvu na akili tu,” alisema.
“Tulichokuwa tunataka ni kuhakikisha tunatengeneza video nzuri nyumbani hata tukifanikiwa kimataifa watu wajue jamaa ameendelea tu ila alianzia nyumbani ndio tunachopambania,watu wa nje wahitaji kufanya kazi na sisi.”
Video ya wimbo huo iliongozwa na Hanscana.

Timbulo aitaja sababu ya kufuta sauti ya Malaika kwenye wimbo wake mpya

Msanii Timbulo amefunguka sababu iliyomfanya afute sauti ya Malaika na kumweka Nay Lee kwenye wimbo wake mpya wa ‘Ngomani’.

http://hamisishehe.blogspot.com
 
Muimbaji huyo amesema kuwa sababu kubwa iliyosababisha ni kuwa busy kwa Malaika kwa madai ya kutoweza kutokea kwenye video ya wimbo huo kwa sababu zake binafsi.
“Nilimshirikisha Malaika kwenye audio na alifanya vizuri lakini baadaye ilipofika muda wa kushoot video lakini siku hiyo akasema hatoweza kuja kwa sababu zake private,” amemuambia mtangazaji wa Fadhila FM ya Masasi, Dj Magasha.
“Video ilikuwa inahusisha watu wengi na tusingeweza kuisitisha kwa ajili yake tukaamua kumtafuta mtu mwingine aliyefiti kwenye hiyo ambaye ni Nay Lee,” ameongeza.
Aidha Timbulo ameendelea kwa kusema kuwa baada ya kumaliza kushoot video hiyo walirudi studio na wakaamua kuifuta sauti ya Malaika iliyokuwa kwenye wimbo huo na kuingiza upya sauti ya Nay Lee kwa sababu alifanya vizuri zaidi.

Zari awapa makavu wabaya wake

Ni muda mrefu mahusiano ya Diamond na Zari yameelezwa kutokuwa mazuri kutokana na muimbaji huyo kuhusishwa kutoka na warembo wengine.


hamisishehe


Kuna tetesi nyingi sana zimevuma kwenye mitandao ya kijamii hivi karibuni zikiwahusu Diamond na Zari.
Huku tetesi hizo zikimhusisha Diamond kusaliti mahusiano yake kwa kutoka na warembo wengine akiwemo Hamisa Mobetto na mrembo aliyetumika kwenye video ya wimbo wa ‘Kwetu’, Irene.
Kupitia mtandao wa instagram wa Zari ameandika ujumbe unaoonekana kuwalenga watu wanaomfuatilia na wasioyatakia mema mahusiano yao. “When your self made, it’s hard to break you no matter how hard they may try. I made me and the only person that can break me is ME not anybody. Ladies now wear this crown👑 and put them heels👠 on and keep it moving. Good night😘,” ameandika Zari.
hamisishehe
Hata hivyo wawili hao wanatarajia kupata mtoto pili wa kiume muda wowote kuanzia mwezi Disemba mwaka huu.

Wizkid kutumbuiza kwenye Fiesta ya Mwanza Jumamosi hii

Staa wa Nigeria, Wizkid, amethibitishwa kuwa atatumbuiza kwenye show ya Fiesta, Mwanza mwishoni mwa wiki hii.


Clouds FM wamethibitisha kumdondosha hitmaker huyo wa ‘Shabba’ Jumamosi, August 20.
“Kituuuuuuu #DealDone kwa mara ya kwanza ndani ya Mwanza #StarBoY wako @wizkidayo utatapata kumshuhudia LIVE juu ya jukwaa la #Fiesta2016 #Imooooo,” wameandika Clouds.
Hii itakuwa mara ya pili muimbaji huyo anakuja Tanzania. Mwezi October mwaka jana alitumbuiza kwenye viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam

source:bongo5 

Sare za polisi zawaponza wasanii wa Orijino Komedi, kuburuzwa Mahakamani

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam kuwachukulia hatua wasanii wa Kundi la Orijino Komedi kwa kuvaa mavazi yanayoshabihiana na sare za polisi.


Akiongea na Clouds FM Msemaji wa Polisi, Advera Bulimba ameeleza kuwa wanatoa onyo kali kwa mtu ama kikundi chochote kuacha kutumia mavazi yanayofanana na sare zinazovaliwa na majeshi ya ulinzi na usalama hapa nchini na atakayebainika hawatasita kuchukua hatua kali za kisheria dhidi yake.
“Jeshi la Polisi linawashikilia wasanii wa Kikundi cha Orijino Komedi kwa kuvaa sere za polisi, hilo moja kwa moja ni kosa kisheria na tayari Jeshi la Polisi Kanda maalum ya Dar es salaam limechukua hatua ya kuwakamata baada ya kukamilisha taratibu zote za kisheria wasanii hao watafikishwa Mahakamani. Kufanya hivyo ni kosa, na watuhumiwa wanatakiwa washughulikiwe kwa mujibu wa sheria za nchi yetu,” alisema Advera.
Wasanii hao wa Kundi la Orijino Komedi walivaa sare hizo katika harusi ya mchekeshaji mwezano Masanja Mkandanizaji.

source:bongo5

Picha: Warembo kwenye video mpya ya Alikiba ni hatari

Alikiba yuko mbioni kuachia silaha yake mpya. Staa huyo wa ‘Aje’ ameonjesha kidogo kile kitakachoonekana kwenye video ya ngoma yake mpya, na mashallah itakuwa na warembo haswaaa.

Staa huyo ameshare picha akiwa mbele ya jumba la kifahari na warembo wanane jijini Johannesburg, Afrika Kusini alikokuwa huko mwezi uliopita.

source:bongo5

Tuesday 16 August 2016

Nimeshakuwa sasa, kiukweli nina kiu ya mume – Johari

Msanii wa filamu, Johari Chagula amefunguka kwa kusema kuwa kwa sasa ana kiu yakumpata mume sahihi ambaye ataingia naye kwenye maisha ya ndoa.


Johari
Mwigizaji huyo ambaye ni mama wa mtoto mmoja, amesema umri wake kwa sasa unamruhusu kuingia kwenye maisha ya ndoa
“Mimi ni mwanamke kamili, ni mtu mzima. Nimeshakuwa sasa, kwahiyo kiukweli nina kiu ya mume,” Johari aliliambia gazeti la Mtanzania. “Mungu akinipa mume bora, nitaolewa. Sitaki kuzungumzia sana mambo yaliyopita, lakini muhimu kwa sasa ni mume,”
Mbali na hayo mwingizaji huyo amewataka kukaa mkao wa kula kwa ajili ya filamu yake mpya ambayo amewashirikisha wasanii wachanga kutoka mkoani Mwanza.

Harmonize: Nivae dela ndio mseme simkopi Diamond?

Shutuma kuwa amekuwa akimuiga bosi wake Diamond, zimemchosha Harmonize na sasa ameamua kujibu.





Baada ya video ya wimbo Inde alioshirikishwa na Dully Sykes kutoka, mashabiki ndio wamezidi kuendelea kusisitiza kuwa msanii huyo anamuiga kwa kiasi kikubwa Diamond.
Harmonize ambaye mara nyingi amekuwa akisisitiza kuwa ndivyo yeye alivyo na yeye sasa ameonekana kuchoshwa na malalamiko ya mashabiki hao ambapo amejikuta akiandika ujumbe wenye utata kwenye Instagram:
Mhhh copy! copy! copy!….. mwisho wa siku hata ukinya utaambiwa kunya kama wewe usimcopy@diamondplatnumz ebwana mzee#simbaa video ijayo wacha nianze kuvaa Dera maana nguo zote ushazivaa 😃😃😃#INDE in my BIO though
😊