Thursday 11 August 2016

Wastara Amnasa Kigogo Morogoro


IMEVUJA! Safari za mara kwa mara mkoani Morogoro, zinazofanywa na staa wa filamu za Kibongo, Wastara Juma zinadaiwa kuchangizwa baada ya kumnasa kigogo mmoja mkoani humo.
Chanzo makini kililiambia Risasi Mchanganyiko kuwa muigizaji huyo amempata mfanyabiashara na kiongozi wa serikali mkoani humo, kitu kinachomfanya afanye safari zaidi ya mara nne kwa mwezi.
“Yaani siku hizi Wastara hatulii Dar ilipo familia yake, amekuwa akisafiri Morogoro kila kukicha, yaani hivi sasa ni mapenzi motomoto, lakini ni kwa siri sana hataki ijulikane,” kilisema chanzo chetu hicho.
Baada ya kuunyaka ‘ubuyu’ huo, paparazi wetu alimtafuta Wastara na alipopatikana, alikana taarifa hizo na kudai safari zake za mara kwa  mara mkoani humo ni kwa vile huko ni nyumbani kwao.
“Hizo habari siyo kweli, watu wanapenda tu kuongea, Morogoro huwa naenda kwa sababu ya mambo mawili, kwanza kule ndiko nilikozaliwa hivyo huwa naenda kuwaona ndugu zangu na pili huwa naenda kwa sababu nina kituo cha kulelea watoto yatima, kwa hiyo huwa naenda kuwaangalia,” alisema Wastara.
sourse:ijumaa weekend

Related Posts

Wastara Amnasa Kigogo Morogoro
4/ 5
Oleh

Subscribe via email

Like the post above? Please subscribe to the latest posts directly via email.