Thursday 11 August 2016

Dr mwaka Ajisalimisha Polisi


Siku chache baada ya Polisi wa Dar es Salaam kutangaza kumsaka mmiliki wa iliyokuwa kliniki ya tiba asilia ya Foreplan, Juma Mwaka ‘Dk Mwaka’ kwa agizo la Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Hamis Kigwangallah, tabibu huyo ameamua kujisalimisha polisi.

Dk Kiwangallah alitoa agizo hilo siku sita zilizopita baada ya kutembelea kliniki hiyo kwa mara ya pili. Dk Mwaka alijisalimisha jana saa nne asubuhi katika Kituo cha Kikuu cha Polisi, jijini Dar es Salaam na kuhojiwa kwa saa kadhaa kabla ya kuachiwa kwa dhamana.

Msako wa Dk Mwaka unachagizwa na madai ya ukiukwaji wa agizo la Serikali la kuendelea na utoaji wa tiba licha ya kufungiwa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, Salum Hamdani alisema jana kuwa baada ya kujisalimisha muda huo, alihojiwa na kuachiwa kwa dhamana lakini akatakiwa kuripoti leo kwa mahojiano zaidi.

“Kuhusu kupelekwa mahakamani, ni mpaka jeshi la Polisi litakapomaliza kukusanya ushahidi na kumkabidhi DPP ambaye atautumia kufungua kesi,” alisema.

Related Posts

Dr mwaka Ajisalimisha Polisi
4/ 5
Oleh

Subscribe via email

Like the post above? Please subscribe to the latest posts directly via email.